Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amepigilia msumari sakata la baadhi ya wanaharakati kutaka wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito shuleni, warudi kuendelea na masomo baada ya kujifungua.
Akizungumza na wananchi wa Bagamoyo wakati wa uzinduzi wa Barabara ya Msata- Bagamoyo, Rais Magufuli amesema serikali yake haiwezi kutoa elimu kwa wazazi bali atatoa elimu kwa wanafunzi ambao kweli wana nia ya kusoma na siyo kufanya masihara.
Rais Magufuli, amesema wakati wa utawala wake, hawezi kuruhusu wanafunzi wazae kisha warudi shuleni kwani akifanya hivyo, itafika hatua mwanafunzi anabeba ujauzito mara mbili au tatu kisha anarudi shuleni.
Akaongeza kwamba mwanafunzi akishapata ujauzito, ni bora akajifunze masomo ya ufundi Veta, au ufundi cherehani au akasome kwenye shule za binafsi lakini siyo shule za serikali na kuongeza kwamba serikali itakuwa na misimamo mikali dhidi ya NGO zinazotetea mambo kama hayo, ya ushoga na matumizi ya madawa ya kulevya.
WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/
FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublishers/
TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari
INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpublishers/
Visit https://globalpublishers.co.tz/, Subscribe /c/uwazi1
Kupata video nyingine za aina hii, subscribe kwenye chanell yetu kwa kubofya…
/c/uwazi1/c/uwazi1/c/uwazi1
WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/
FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublishers/
TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari
INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpublishers/